[Latest Updates]: Dkt. Kiruswa: Wizara Kuendelea Kuwaunganisha Wachimbaji Wadogo wa Madini na Taasisi za Fedha

Tarehe : May 8, 2023, 11:55 a.m.
left

Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa amesema Wizara imejipanga kuendelea kuwawezesha na taasisi za fedha wachimbaji wadogo wa madini ili wapatiwe mikopo kwa lengo la kuchimba kwa tija na kukua kutoka kwenye uchimbaji mdogo kwenda wa kati na hatimaye kwenda kwenye uchimbaji mkubwa.

Dkt. Kiruswa amesema hayo wakati akikagua mabanda ya maonyesho katika Kongamano la Mkutano Mkuu wa FEMATA linaloendelea jijini Mwanza ambapo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kasimu Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kilele chake.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Adam Malima amelipongeza Shirikisho la Wachimbaji Wadogo wa Madini Tanzania (FEMATA) kwa maamuzi ya kufanya Kongamano la kwanza mkoani humo.

"Sisi kama mkoa wa Mwanza tunaipongeza FEMATA kwa maamuzi ya kuleta Kongamano hili jijini Mwanza, tunawahakikishia ulinzima na usalama katika kipindi chote mkiwa hapa mwanza," amesema Malima.

Naye, Rais wa FEMATA John Bina amesema zaidi ya mada 22 zimewasilishwa na wataalamu mbalimbali kwa wachimbaji wadogo wa madini katika Clinic ya Madini inayoendelea katika viwanja vya Rock City Mall Jijini Mwanza.

 

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals