[Latest Updates]: Waziri Biteko aanza kutatua mgogoro kati ya Mzee Mchata, Kampuni ya Mantra

Tarehe : Jan. 28, 2019, 11:01 a.m.
left

Na Asteria Muhozya,

Waziri wa Madini, Doto Biteko leo Januari 28, amekutana na Mzee Eric Mchata na Kampuni ya madini ya Uranium ya Mantra Tanzania kwa lengo la kutatua mgogoro uliopo baina ya pande hizo mbili.

Kikao hicho, kinafuatia malalamiko yaliyowasilishwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli Januari 22 na  Mzee Mchata wakati wa mkutano wa Kisekta ulioshirikisha wachimbaji wadogo na wadau wa madini uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Wakati akisikiliza kero za wachimbaji na wadau wa madini walioshiriki kikao hicho, Rais Magufuli alipokea kero ya Mzee Mchata aliyemweleza kwamba amekuwa na mgogoro na kampuni hiyo kwa kipindi cha takribani miaka 12 na bado hajapata suluhu.

Akijibu kero iliyowasilishwa na Mzee Mchata, Rais Magufuli aliitaka Wizara ya Madini kuhakikisha mgogoro huo unafikia mwisho.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals