[Latest Updates]: Wadau wa Madini Washauriwa Kuungana Ili Kuzalisha kwa Tija

Tarehe : Sept. 22, 2020, 11:07 a.m.
left

Tito Mselem na Steven Nyamiti

Waziri wa Madini Doto Biteko amewashauri Wadau wa Madini wa Mkoa wa Geita kuungana na kutengeneza Kampuni ya pamoja ili kuongeza tija katika shughuli zao.

Ushauri huo, ameutoa mara baada ya kutembelea Maonesho ya Tatu ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye Sekta ya Madini yanayoendelea Mkoani Geita.

Wakati huo huo, Waziri Biteko ametoa pongezi kwa waandaji wa Maonesho hayo ambayo mwaka huu zaidi ya kampuni 420 zinashiriki.

Vilevile, Waziri Biteko ametoa Wito kwa taasisi za Kibenki kuendelea kuwalea Wachimbaji Wadogo na Wafanyabiashara ya Madini kwa kuwapa mafunzo pamoja na mikopo ili wazalishe kwa faida.

Naye, Mkurugenzi wa Mikopo kwa Wajasiliamali Wadogo wa NBC Elibariki Masuke, amesema Benki ya NBC Mkoa wa Geita imetoa mkopo wa zaidi ya Shilingi bilioni 4.4 kwa Wadau wa Sekta ya Madini mkoani humo ili kuwaongezea uwezo katika shughuli zao.

Hayo aliyasema mbele ya Waziri Biteko alipotembelea banda la la benki ya NBC katika Maonesho ya Tatu ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye Sekta ya Madini yanayoendelea mkoani Geita.

Imeelezwa kuwa, wanufaika wa mikopo hiyo ni pamoja na Wachimbaji Wadogo, Wafanyabiashara ya Madini na Wachenjuaji wa Madini wa Mkoa wa Geita.

"Sisi kama Benki ya NBC tumeanza kutoa mafunzo kwa Wadau wa Madini hususan Wachimbaji Wadogo wa dhahabu na Wafanyabiashara ya dhahabu ili kuwajengea uwezo wa namna bora ya kuwekeza katika Sekta ya Madini", alisema Masuke.

Pamoja na mambo mengine, Masuke amesema Banki ya NBC imekuwa Mdau Mkubwa kwenye Sekta ya Madini  ambapo mpaka sasa kuna taratibu zinawekwa sawa ili mikopo mikubwa zaidi ianze kutolewa kwa Wadau wa Sekta ya Madini kote nchini.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals