[Latest Updates]: Wachimbaji wadogo kutunukiwa Vyeti vya Uhifadhi wa Mazingira

Tarehe : Jan. 28, 2019, 5:21 p.m.
left

Na Nuru Mwasampeta,

Waziri wa Madini, Doto Biteko amekutana na Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Samuel Gwamaka Mafwenga, ofisini kwake jijini Dodoma.

Biteko ameshukuru Dkt. Mafwenga kwa kuonesha nia ya kuwasaidia wachimbaji wadogo kupata cheti cha mazingira baada ya kubainisha njia bora za kuwawezesha wachimbaji wadogo kupata uelewa juu ya uhifadhi wa mazingira.

Akizungumza katika kikao hicho kilichofanyika Januari 28, 2019, Dkt. Mafwenga amesema kutokana na mwamko mkubwa iliyonayo Serikali wa kuwasaidia wachimbaji wadogo kukua na kufanikiwa katika sekta ya uchimbaji mdogo wa madini, Nemc itajikita katika kuhakikisha inashirikiana na wizara katika kuhamasisha na kuelimisha wachimbaji wadogo juu ya umuhimu wa uhifadhi wa mazingira.

Aidha, amebainisha kuwa, kutokana na vigezo vya awali ambavyo viliwafanya wachimbaji wadogo kutokupewa cheti cha mazingira zitaboreshwa na kuwawezesha kupata cheti hicho.

Amesema, wachimbaji wadogo watapaswa kusajili miradi yao katika Ofisi za Kanda za Baraza la Hifadi la Mazingira  ambao watakagua miradi hiyo na baada ya kujiridhisha watawapatia vyeti hivyo.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals