[Latest Updates]: Wizara ya Madini Yakabidhi Vyeti kwa Wahitimu 28 wa Mafunzo ya Utunzaji Mazingira na Ufungaji wa Migodi

Tarehe : Feb. 23, 2024, 8:33 p.m.
left

WIZARA YA MADINI YAKABIDHI VYETI KWA WAHITIMU 28 WA MAFUNZO YA UTUNZAJI MAZINGIRA NA UFUNGAJI MGODI

 Ifikapo Machi Jukwaa la Kiserikali (IGF) Kuendesha mafunzo kuhusu kodi za Madini 
 
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Augustine Olal, ametoa Vyeti kwa Wahitimu 28 wa Mafunzo ya Utunzaji Mazingira na kufunga migodi  walioshiriki mafunzo hayo.

Amekabidhi vyeti hivyo leo Februari 23, 2024 katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Rafiki Hotel Jijini Dodoma.

Amesema dhumuni la mafunzo hayo lilikuwa ni kuongeza ujuzi, maendeleo na umahiri unaohitajika kwa utawala bora wa kijamii wa mazingira katika Uchimbaji Madini, ikisisitizwa juu ya kufungwa kwa Migodi na usimamizi wa mazingira.

Olal amesema, katika siku nne za mafunzo  yalijikita katika mada muhimu kama vile Chombo na majibu ya maandalizi ya Dharura, Usimamizi wa maji,  Udhibiti wa taka, Ufungaji wa Migodi na Uchimbaji baada ya uchimbaji.

Aidha, Olal amesema,  Wizara iko tayari kushirikiana na Jukwaa la Kiserikali (IGF) katika kuwajengea uwezo watanzania  katika sekta ya Madini na miradi mingine ambayo ni muhimu kwenye Wizara ya Madini na Sekta ya Madini kwa ujumla.

“Tunapohitimisha mafunzo haya, tuendeleze maarifa na uzoefu uliopatikana ili kuchangia maendeleo endelevu ya sekta yetu ya Madini na uhifadhi wa hazina zetu za asili zikiwemo juhudi zetu zifungue njia kwa wingi zaidi katika uchimbaji Madini unaozingatia mazingira na uwajibikaji nchini Tanzania,” amesema Olal.

Awali, Kamishna wa Madini Dkt. AbdulRahman Mwanga,  amewashukuru na kuwapongeza wakufunzi kwa kutoa mafunzo stahiki na kuwashukuru washiriki wote kwa kushiriki kikamilifu na kusisitiza kuwa mafunzo haya yawe endelevu ili kuongeza wataalam katika tasnia hii ya Madini. 
 
#Vision2030MadininiMaishanaUtajiri#

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals