[Latest Updates]: Leseni za Migodi Mikubwa Kutolewa Karibuni

Tarehe : Feb. 27, 2019, 2 p.m.
left

Na Asteria Muhozya, Dodoma

Serikali kupitia Wizara ya Madini inakamilisha taratibu za utoaji wa Leseni kwa Migodi Mikubwa ambazo hazijawahi kutolewa nchini, huku migodi hiyo ikitarajiwa kuanzishwa hivi karibuni.

Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila alipokutana na viongozi wa Jumuiya ya Watendaji Wakuu wa Taasisi Binafsi ofisini kwake, jijini Dodoma.

Viongozi hao walikutana na Prof. Msanjila Februari 26, kwa lengo la kujitambulisha, kuelewa shughuli za serikali upande wa sekta ya madini, kupata uelewa kuhusu mabadiliko ya Sheria ya Madini na namna pande hizo mbili zinavyoweza kushirikiana katika kuendeleza sekta husika.

Prof. Msanjila aliwakaribisha viongozi hao kwenye sekta ya madini huku akiwataka kuzishawishi kampuni mbalimbali kuwekeza nchini hususani katika shughuli za uongezaji thamani madini na kueleza kuwa, suala hilo ni miongoni mwa maeneo ambayo serikali inayapa kipaumbele ikiwemo ujenzi wa vinu vya kusafisha na kuyeyusha madini.

Akizungumzia Sheria Mpya ya Madini ya Mwaka 2017, Prof. Msanjila amesema hakuna tatizo lolote katika utekelezaji wa sheria na kueleza kuwa, serikali kupitia wizara ya madini inapokea wawekezaji wengi wenye utayari na nia ya kuwekeza nchini huku utekelezaji wa sheria hiyo ukiwa si kikwazo na kuongeza kwamba, “hakuna mahali ambapo serikali inatengeneza sheria kwa ajili ya kumkandamiza mfanya biashara”.

“Hakuna tatizo lolote kwenye sheria ya madini. Hata wageni huwa tunakaa nao tunawaelimisha na wanatuelewa vizuri.  Kama kuna dosari ni vitu ambavyo tunaweza kuvirekebisha na tayari tumekwishakufanya hivyo kwa baadhi ya maeneo,” alisema Prof. Msanjila.

Aidha, katika kikao hicho Prof. Msanjila alitoa ushauri kwa viongozi hao kujitangaza zaidi kuhusu kazi zao huku akiwataka kutafuta wasaa kwa ajili ya pande hizo mbili kukutana ili wizara iweze kutoa elimu zaidi kwa Jumuiya hiyo kuhusu sekta ya madini ikiwemo fursa za uwekezaji zilizopo.

Pia, Prof. Msanjila alisema kuwa suala la kuaminiana linaweza kujengwa huku akiwataka watanzania kuwa wazalendo na namna wanavyotumia fedha za umma. Prof. Msanjila alizungumzia jambo hilo baada ya mmoja wa viongozi hao kueleza kuwa, bado kuna hali ya kutokuaminiana baina ya serikali na taasisi binafsi.

Kwa upande wake, mmoja wa viongozi wa jumuiya hiyo, Francis Nanai ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited amemweleza Prof. Msanjila kuwa, kama viongozi wa umoja huo, wamezipokea changamoto zilizotolewa kwao na Prof. Msanjila ikiwemo ushauri wa kukutana na wizara kwa lengo la kupata ufafanuzi na elimu  zaidi  kuhusu sekta ya madini.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals