[Latest Updates]: Rafiki Briquettes Yawa Kivutio Kikubwa Kwa Uchomaji Nyama Arusha

Tarehe : March 8, 2025, 3:09 p.m.
left

Nishati ya Rafiki Briquettes  inayozalishwa na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO)  ndio muwezeshaji mkubwa wa nishati safi inayotumika hapa Mkoani Arusha kwenye usiku wa nyama choma leo Machi 07, 2025.

Tukio hili la uchomaji nyama linafanyika kwenye makutano ya barabara eneo la Clock Tower ikiwa ni sehemu ya shamrashamra za maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake tarehe 8 Machi.

Kitaifa maadhimisho haya yanafanyika mkoani Arusha.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Ndugu Paul Makonda amevutiwa na nishati hii na kuahidi kuitumia katika matukio yote ya umma katika Mkoa huu.

Rafiki Briquettes  ni nishati rafiki kwa mazingira na isiyokuwa na madhara ya kiafya kwa watumiaji kwani haitoi moshi kama ilivyo kwa mkaa unaotokana na miti pamoja na kuni.

Nishati hii ina uwezo wa kuivisha na kuchoma nyama na vyakula vinginevyo katika viwango stahiki.

Taasisi nyingi za elimu, Jeshi la Magereza na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) zinatumia nishati ya Rafiki Briquettes kupikia.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals