[Latest Updates]: Ujumbe Kutoka Burkina Faso Watembelea STAMICO

Tarehe : Nov. 22, 2024, 6:55 p.m.
left

Ujumbe kutoka Burkina Faso umetembelea Shirika la Madini la Taifa  (STAMICO) na kufanya  Kikao kazi ili kujifunza  kuhusu sekta ya madini,leo  Novemba 22, 2024

Katika kikao kazi hicho 
STAMICO imeeleza kwa kina namna serikali inavyoshiriki katika uvunaji wa rasilimali madini kwa kutoa wasilisho kuhusu inavyosimamia na kuendesha miradi yake ili kuhakikisha  inaleta tija kwa Taifa

Akiongea kwa upande wa STAMICO  Kaimu Mkurugenzi Mtendaji  Bw. Mudrikati Kiobya  amesema ili nchi iwezekunufaika na rasilimali  madini ni vizuri Serikali kushiriki kwenye uchimbaji, kuwawezesha wachimbaji wadogo ili waweze kuendeleza rasilimali hizo.

Naye kiongozi wa Ujumbe huo kutoka Burkina Faso  Bw.  HIEN Jonas, amesema  wamefanya ziara ya kujifunza kuhusu STAMICO ili kuweza kutumia uzoefu huo kufanya uwekezaji katika sekta ya madini nchini kwao. 

Ameeleza kuwa nchini kwao hawana taasisi ya Serikali  inayojihusisha na uvunaji wa rasilimali  madini bali wana taasisi tofauti zinazowasimamia wachimbaji japokuwa wameanzisha taasisi ya serikali (Refinery )kwa ajili ya kununua na kusafisha dhahabu.

Ametumia fursa hiyo kuishukuru Serikali   kupitia STAMICO kwa maelezo mazuri yaliyoendana na matarajio yao kwani wameweza kujifunza jinsi ya  kuwasaidia wachimbaji wadogo,  sambamba na kuendesha miradi ikiwemo  mradi wa kusafisha dhahabu na miradi mingine.

Utendaji bora wa STAMICO  umeendelea kuwavuta mataifa  mbalimbali  kuja kujifunza namna Serikali  inavyoweza kusimamia na kushiriki  katika  uvunaji  wa rasilimali madini  kwa manufaa ya taifa lake.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals